UGONJWA WA MALARIA NI NINI?

Malaria ni katika maradhi yanayosumbua sana na kusababisha maradhi ya watu wengi sana duniani. Malaria ni katika maradhi yanayopatikana katika maeneo yenye joto, hususani maeneo yenye uoto wa kitropiki. Miongoni mwa maeneo ambayo yanasumbuliwa zaidi na malaria ni bara la Afrika.

 

Inakadiriwa kuwa mila mwaka watu milioni 210 (210,000,000 wanapata malaria kila mwaka na kati ya hao watu laki nne na elfu arobaini (440,000) wanakufa kwa ugonjwa huu kila mwaka na wengi wao ni watoto walio chini ya umri wa miaka mitano.

 

Mpaka sasa bado hakuna chanjo ya malaria ijapokuwa wataalamu wa afya wanajitahidi kuitafuta chanjo yake. Miili inaweza kutengeneza njianjo yao wenyewe japo ni ya muda na sio ya kuzuia malaria kabisa isipokuwa inaweza kupunguza athari za ugonjwa huu. Na hii ndio maana matu anaweza kuishi na malaria kwa muda mrefu bila ya kuumwa hasa.