5. HOMA YA BONDE LA UFA (RVFD)

Homa hii inapatikana katika maeneo ya bonde la ufa barani Afrika na na Mashariki ya kati. Historia inaonyesha kuwa mnamo mwaka 1977 na 1978 mamilioni ya watu waliathirika na maradhi haya na maelfu ya watu walifariki kwa ugonjwa huu.

 

Homa ya bonde la ufa mwanzo kabisa ilifahamika kuwa inaathiri mifugo, ila kwa sasa tunatambua kuwa binadamu nae anaweza kuupata ugonjwa huu. msambazaji mkuu wa maradhi haya ni mbu aina ya Aedes, pindi anapomng'ata mtu huweza kubeba vimelea na kusambaza.

 

Dalili za homa hii pia hufanana na baadhi ya maradhi tulioyataja hapo juu. Dalili hizo ni:-homa, udahifu, maumivu ya mgongo, kuhisi kizunguzungu pamoja na kupungua uzito. Mara cache sana ugonjwa huu unaweza kupelekea hemorrhage hali inayopelekea kutokwa na damu aua meningoencephalitis hali inayopelekea kuvimba kwa ubongo.