HISTORIA YA MAISHA YA UTOTONI YA MTUME MUHAMMAD (S.A.W)

MAISHA YA UTOTONI YA MTUME S.

HISTORIA YA MAISHA YA UTOTONI YA MTUME MUHAMMAD (S.A.W)


MAISHA YA UTOTONI YA MTUME S.A.W
Ilikuwa ni tamaduni kwa waarabu waishio mjini kuwapeleka watoto wao wachanga vijijini wakalelewe ili wapate ukakamavu, wajifunze lugha vyema na pia kuwaepusha na magonjwa ya miripuko yanayotokea mijini. Hivyo Mtume s.a.w alichukuliwa na Halima bint Dhuaib kutoka katika kabila la bani Sa'ad bin Bakar. Mume wake aliitwa Al-Harith bin 'Abdul'Uzza pia alitambulia kwa jina la Abi Kabshah.

Halima anasimulia kuwa ulikuwa ni wakati wa ukame sana hususana sehemu ambay alikuwa akiishi yeye na watu wao. Mvua zilikata, wanyama hawakuweza kutoa maziwa kwa ukame uliopo. Wanyama hawakuweza kushiba. Shakula pia kilikuwa ni taabu, lakini tumaini lao lilikuwa ni kusubiria mvua inyeshe. Wakati huo walitoka watu waende mjini kwenda kutafuta watoto wa kuwalea ili waweze kupata kipato kama ujira wa kulea na kunyonyesha watoti hao kama ilivyokuwa ni kawaida yao. Alikuwepo kwenye msafara huu Halima na mume wake.

Bi Halima akiwa amepata punda wake aliyeonekana ni dhaifu sana na mumewe alikuwa amepanda ngamia ameye hakuwa ni mwenye kutoa maziwa. Walifika Maka na wakaanza kutafuta watoto wa kuwanyonyesha. Anaeleza bi halima kuwa katika msafara ule walotoka watu wote walifika kwa mama yake Mtume na kuelezwa kuwa mtoto huyu ni yatima, basi wote wakakataa kumchukuwa Muhammad kwenda kumlea kwa kuhofia wazazi wake hawataweza kulipa gharama kwani mtoto ni yatima.

Msafara huu uliendelea kuzungua Makkah kutafuta watoto wa kuwalea, halimaye bi Halima hakibahatika kupata mtoto, hivyo akashauriana na mumewe kuwa arudi kule kwa mtoto yatima kwani anaona vibaya kurudi mtupu pila ya kuwa na mtoto. Basi mumewe akakubali, na hapo bi Halia akarudi na kumchukuwa mtoto muhammad (s.a.w). na maajabu ndo yakaanza hapa kama vile bi Halima anavyotueleza, Nitataja kwa ufupi zaidi mambo haya yalotokea.

Anaeleza bi Halima kuwa alipombeba mtoto badi alipofika kwenye hema lao aloshangaa kuona maziwa yamejaa, kwa hakika hii ni ajabu kwake kwani hata mtoto wake alikuwa akikosa usingizi usiku kwa uchache wa maziwa. Lakini leo anakuwa na maziwa na kumtosha mtot muhammad pamoja na mtoto wake. Kwa hakika walinyonya watoto hawa wawili mpaka wakashiba na kulala.

Bi halima anasimulia kuwa mume wake alipotoka kwenda kumuangalia ngamia wake alishangaa kuona ngamia ana maziwa ya kutosha, alikamua maziwa kutoka kwenye ngamia wake wakanywa na kushiba. Hii pia ni ajabu aloishuhudia Bi halima baada ya kumchukuwa kijana Mhammad kwa ni hapo mwanzo ngamia wao hakuweza kutoa hata tone la maziwa ya kuweza kunywa, lakini leo ngamia huyu anatoa maziwa ya kuweza kushiba watu wa familia hii na kuyabakisha. Bi Halima anasimula kuwa asubuhi ya siku ilofata mume wangu aliniambia ' hakikahalima umechukuwa mtoto mwenye kubarikiwa' nikamjibu 'nami natarajia iwe hivyo'.

Siku ilofata safari ya kurudi kutoka maka kwenda kwao ilianza. Katika msafara huu walishangaa kumuona punda wa halima amebadilika kwani amekuwa na nguvu na ameongeza uwezo wa kukimbia. Ilifikia wakati wnzie wakawa wanamwmbia nenda kipolepole ewe Halima kwa hakika huyu si yule pinda ulokuja ne. Ukweli ni kuwa punda ni yuleyule lakini Allah ameta miujiza yake hapa.

Walipofika nyumbani walishangaa kuona mifugo yao inarudi kutoka malishoni ikiwa imeshiba sana, wakati kulikuwa na ukame mkubwa sana. Mifugo yao iliweza kutoa maziwa mengi. Ilifikia wakati wamiliki wa mifugo wakawa wanawaambia wachungaji wao kuwa wachunge pale anapochungia mchungaji wa bi Halima. Ukweli ni kuwa majani ni yale yale isipokuwa Allah anaweza miujiza yake kwa bi Halima.

Kwa hakika bi Halima aliona miujiza mingi sana, na maisha yake yalibadilika na kuwa na raha na amani to ka amchukuwe mtoto Muhammad (s.a.w). bi Halima anasimulia kuwa mtoto Muhammad alikuwa anakuwa kwa haraka zaidi tofauti na alivyozoea. Bi Halima alimlea mtoto huyu kwa muda wa miaka miwili hata muda wa kumuachisha ziwa ukawadia. Ilikuwa anatakiwa ampeleke mtoto kwa mama yake.

Basi mtoto alipotimia miaka miwili kwa shingo upande bi Halima alimrudisha mtoto kwa mama yake. Huku akiwa haridhiki kwani ameona neema nyingi toka amchukuwe mtto huyu. Alipofika Makkah alimshawishi mamayake amruhusu aweze kurudi nae aendelee kumlea kwa kuhofia mtoto atpata maradhi ya mjini maradhi ya milipuko. Kwa sababu hii mama yake Mtume bi Amina alikubali hivyo bi Halima akaendelea kumlea mtoto huyu. Hvyo Mtume aliendelea kuishi kule na kuendelea kuimarika kimwili na kuwa na afya njema pamoja na kupata ufasaha katika lugha ya kiarabu.


                   

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 311

Post zifazofanana:-

Elimu
Uwanja wa elimu na maarifa Soma Zaidi...

SECONDARY SCHOOL GROGRAPHY FOR FORM ONR
Soma Zaidi...

HUDUMA YA KWANZA KWA ALIYEPATWA NA KWIKWI
Kwikwi sio hatari sana kwa afya, lakini inaweza kuwa hatari zaidi kwa mu aliyefanyiwa upasuaji kwenye tumbo. Soma Zaidi...

Kuepuka Maongezi yasiyo na Maana
12. Soma Zaidi...

Usimamizi wa Haki na haki za binadamu Katika Dola ya Kiislamu
Soma Zaidi...

DUA YA MUUMINI NA DUA YA KAFIRI
DUA YA KAFIRI NA DUA YA MUUMINI. Soma Zaidi...

NAMNA AMBAZO DUA HUJIBIWA
NAMNA AMBAYO ALLAH HUJIBU DUA. Soma Zaidi...

school makataba
1. Soma Zaidi...

MAAJABU YA VIUMBE
MAAJABU YA VIUMBE Dunia ina maajabu sana lakini viumbe wana maajabu pia. Soma Zaidi...

MAANA YA ZAKA NA SADAKA KULUNGA NA KISHERIA PAMOJA NA TOFAUTI ZAO
MAANA YA ZAKA NA SADAKA KULUNGA NA KISHERIA PAMOJA NA TOFAUTI ZAO. Soma Zaidi...

Fahamu vitamini K na kazi zake, vyakula vya vitamini k na athari za upungufu wake
kuhusu vitamini K, wapi tutavipata, ni zipi athari zake na ni zipi kazi zake mwilini. Soma Zaidi...

Dalili Kubwa za kukaribia Siku ya kiama
Soma Zaidi...