Vyakula na vinywaji hatari na vilivyo salama kwa mgonjwa wa kisukari

Hapa utajifunza vyakula hatari kwa mgonjwa wa kisukari, pia utajifunza vyakula salama anavyotakiwa ale mgonjwa wa kisukari, Pia ujajifunza njia za kujikinga na kisukari

Vyakula na vinywaji hatari na vilivyo salama kwa mgonjwa wa kisukari

VYAKULA SALAMA NA HATARI KWA MWENYE KISUKARI
Kisuari ni hali ya mwili kushindwa kudhibiti kiwango cha sukari hivyo kuachia sukari yote kuishia kwenye damu bila ya kuingia kwenye seli ili kutumika maeneo mbalimbali ya mwili. Na hutokea endapo uzalishwaji wa homoni ya insulini utakuwa katika shida. Eidha hutokea kwa sababu homoni ya insulini inayozalishwa si yenye kutosheleza ama mwili wenyewe unashindwa kuitumiahomoni ya insulini. Homoni ya insulin ndio ambayo hudhibiti kiwango cha sukari.



Vipi kisukari hutokea?
Mwili unahitaji sukari kwa ajili ya kuzalisha nishati yaani nguvu. Mwili pia unahifadhi sukari kwa matumizi ya baadaye. Endapo sukari mwilini itakuwa ni nyingi basi homoni ya insulini huzaliwa kwa wingi ili kupunguza sukari iliyozidi n akuihifadhi kwa matumizi yaa baadaye. Na endapo sukari itakuwa ni kidogo mwilili homoni ya insulini huzuiliwa hivyo mwili hutumua sukari iliyohifadhiwa. Kwa kufanya hivi kiwango cha sukari hudhibitiwa.



Sasa endapo kutatokea shida yeyote katika matumizi ya homoni ya insulini mwili utashindwa kuhifadhi sukari pia kuitumia sukari. Hivyo sukari itabakia kwenye damu bila ya kwenda kokote kwa matumizi. Hali hii ikitokea ndipo mtu huambiwa ana kisukari. Kisukari kinaweza kuwa ni kwa muda mfupi kama kwa baadhi ya wajawazito. Pia kinaweza kuwa ni cha kudumu, na hapa tunazungumzia type1 na type 2.



Mtu mwenye kisukari anatakiwa kuwa makini sana katika matumizi ya vyakula na vinywaji. Vinginevyo anaweza kuingia kwenye matatizo makubw aya kiafya. Je unavijuwa vyakula salama kwa nmwemye kisukari? Na je unavijuwa vyakula hatari kwa mwenye kisukari? Endelea na makala hii hadi mwisho:-



VYAKULA SALAMA KWA MWENYE KISUKARI
1. Samaki hasa wale wenye fati kwa wingi kama samlon na sardines
2. Mbogamboga za majani
3. Palachichi
4. Mayai
5. Mbegu za chia
6. Maharagwe
7. Kitunguu thaumu
8. Nyama yandege wafugwao kama kuku
9. Kahawa
10. Vinywaji visivyowekwa sukari
11. Jusi za mbogamboga
12. Usikoboe mahindi, mchele, na mtama
13. Matunda kwa uchache



VYAKULA HATARI KWA MWENYE KISUKARI
1. Nafaka zilizokobolewa
2. Nafaka zilizoongezwa sukari
3. Mikate yenye sukari
4. Nafaka zisizo na kini
5. Mboga zenye chumvi nyingi
6. Mboga zilizoongezwa maziwa
7. Vinywaji vyote vya sukari usitumie mpaka kiwango chako cha sukari kiwe kipo katika udhibiti hata asali epukana nayo kwanza
8. Juisi zilizowekwa sukari ama zenye utamu kama za matunda
9. Vinywaji vya energy (energy drink)
10. Nyama ya kuoka
11. Nyama zenye mafuta mengi
12. Nyama ya ngurue
13. Maziwa fresh
14. Samaki wa kuoka
15. Soda



Njia za kujikinga na kisukari
1. Dhibiti uzito wako. Hakikisha huna uzito w akupitiliza
2. Fanya mazoezi mara kwa mara
3. Kula mlo kamili
4. Punguza misongo ya mawazo
5. Kunywa maji kwa wingi
6. Wacha kuvuta sigara
7. Punguza ama wacha unywaji wa pombe
8. Punguza ulaji wa sukari kwa wingi
9. Pendelea kunywa kahawa
10. Tumia dawa za asili kiasi uwezavyo





                   



Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 279


Download our Apps
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-