Ni yapi mambo yanayoharibu Swaumu na Mambo yanayobatilisha funga

Ni yapi mambo yanayoharibu Swaumu na Mambo yanayobatilisha funga

Yanayobatilisha Funga



Mtu aliyefunga analazimika kujizuilia na vitendo mbalimbali ambavyo hubatilisha funga yake. Mfungaji akifanya moja wapo katika yafuatayo swaum yake itabatilika.


(i)Kula na Kunywa
Ukila au ukinywa chochote kile kwa kudhamiria hata ikiwa ni dawa utakuwa umefungulia. Vile vile ukivuta sigara au chochote kile au ukivuta dawa ya mafua kwa pua utakuwa umefungua. Pia kupitisha chochote puani au masikioni kwa kudhamiria, hata ikiwa dawa utakuwa umefu n gu a.



Ikumbukwe kuwa kujifunguza makusudi katika mwezi wa Ramadhani kwa kula na kunywa bila ya udhuru wowote wa kisharia ni kosa kubwa sana mbele ya Allah(s.w) kwa kiasi ambacho hata kama mtu atafunga umri wake wote hataweza kuilipia hiyo siku moja aliyojifunguza makusudi kama tunavyojifunza katika Hadith ifuatayo:



Abu Hurairah(r.a) ameeleza kuwa Mtume (s.a.w) amesema: Yule anayefungua siku moja ya Ramadhani bila kuwa mgonjwa au kuwa na udhuru mwingine wa kisheria, hata akifunga maisha yake yote hataweza kuilipia funga hiyo. (Ahmad, Tirmidh, Abu Daud, Ibn Majah, Darimi).



Hadith hii inatuasa tusifanyie mas-khara amri za Allah (s.w). Hivyo mtu akijifunguza makusudi ajue wazi kuwa amefanya kosa kubwa ambalo halitasameheka kwa kuilipia tu siku hiyo bali ni lazima pia arejee kwa Mola wake kwa toba ya kweli.



(ii)Kujitapisha Makusudi
Mtu akijitapisha makusudi funga yake itavunjika kutokana na Hadith ifuatayo:
Abu Hurairah(r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: Anayeshindwa kuzuia matapishi halipi. Lakini anayejitapisha makusudi, na alipe. (Tirmidh, Abu Daud, Ib Majah).
Kutokana na Hadith hii kutapika kwa ugonjwa hakufunguzi.



(iii)Kupatwa na Hedhi au Nifasi
Mwanamke akipatwa na hedhi au nifasi hata kama imempata nyakati za mwisho kabla ya jua kuchwa, atakuwa amefungua na atalazimika kuilipia siku hiyo baada ya Ramadhani.



(iv)Kujitoa Manii Makusudi Ukijitoa manii kwa mkono au kwa kubusiana na kukumbatiana mume na mke, au kwa njia nyingine yoyote ile utakuwa umefungua.Kutokwa na manii kwa kuota au kwa njia nyingine isiyokuwa ya makusudi, hakufunguzi.



(v) Kunuia Kula na hali umefunga
Ukinuia kula hata kama hukula swaumu yako itakuwa imebatilika kwa kuwa utakuwa umevunja nguzo moja ya funga - nia.




                   


Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 579

Post zifazofanana:-

Mitume wa uongo
Wafuatao ni baadhi ya wale waliodai utume wakati Mtume (s. Soma Zaidi...

Maandalizi ya maiti: kumuosha, kumkafini ama kumvalisha sanda na kumzika
Soma Zaidi...

DARASA LA AFYA, AFYA YA UZAZI, MARADHI NA LISHE BORA
Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote Soma Zaidi...

GEOGRAPHY NECTA PAST PAPERS REVIEW PAPERR 02
40. Soma Zaidi...

NAMNA YA KUSWALI SWALA YA IJUMAA, JENEZA, SWALA YA JAMAA NA SWALA YA SUNNHA (tarawehe, tahajudi na qiyamu layl)
1. Soma Zaidi...

surat al mauun
SURATUL-MAM'UUN Imeteremshwa Maka, anasimulia Ibn Jurayj kuwa Abuu Sufyan ibn Harb alikuwa na kawaida ya kuchinja ngamia wawili kila wiki, hivyo siku moja yatima mmoja alikuja kwake na kumlilia shida, na hakumsaidia kwa chochote na hatimaye akampiga yat.. Soma Zaidi...

HOMA YA DENGUE, DALILI ZAKE, TIBA YAKE, CHANGO YAKE NA INA SABABISHWA (AMBUKIZWA) NA MBU GANI
Homa ya dengue hupatikana sana Afrika, Asia na baadhi ya maeneo ya Caribbean. Soma Zaidi...

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Nuhu(a.s)
(i) Tuanze kulingania kwa Tawhiid ' kumjua Allah(s. Soma Zaidi...

MARADHI YASABABISHWAYO NA HALI ZA MAISHA
Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote Soma Zaidi...

KITABU CHA MATUNDA
Jifunze sifa na aina za matunda, vijuwe viruturubisho Soma Zaidi...

Hii ndio namna ya kuswali kama alivyoswali Mtume s.a.w
Mtume (s. Soma Zaidi...

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Ismail(a.s)
Kutokana na Historia ya Nabii Ismail(a. Soma Zaidi...