Aina ya talaka zisizo rejewa

2.

Aina ya talaka zisizo rejewa

2.Talaka Isiyorejewa
Talaka isiyorejewa ni ile ambayo mtu hawezi tena kumrejea mkewe hata kama watasuluhishana kabla ya eda au baada ya eda. Kuna ama kuu mbili za talaka zisizorejewa:
(a)Talaka Tatu.
(b)Talaka ya Li'aan.



(a)Talaka tatu
Talaka tatu zinapatikana kwa kutamka dhamira ya kumuacha mke mara tatu katika kila twahara ndani ya twahara tatu za eda. Vile vile zitahesabika talaka tatu kama mume katika muda wa ndoa yao amewahi kutoa talaka rejea mbili kwa kipindi kimoja cha eda au vipindi tofauti ambapo walipatana na kurejeana. Pia kama mtu na mkewe waliwahi kuvunja ndoa mara moja kwa talaka mbili kisha mara zote hizo mbili walipatana kufunga ndoa tena watakapopeana talaka katika ndoa yao hii ya mwisho, talaka hiyo itahesabika kuwa ni talaka ya tatu.


Ni kinyume kabisa na sheria ya Kiislamu kutoa talaka tatu mfululizo katika kikao kimoja au katika twahara moja kwa matamshi. Wanachuoni wengi wamekubaliana kuwa talaka ya namna hiyo itahesabiwa kuwa ni talaka moja. Waislamu wanaofanya hivyo, wajue kuwa huko ni kuzifanyia mzaha aya za Mwenyezi Mungu na kuvuka mipaka ya Mwenyezi Mungu. "Na anayeruka mipaka ya Mwenyezi Mungu basi amejidhulumu nafsi yake " (65:1).



Uislamu umekataza vikali mchezo wa kutoa talaka tatu kwa mpigo kama tunavyojifunza katika hadithi: Mahmuud bin Labiid (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu alieelezwa juu ya mtu aliyetoa talaka tatu mfululizo kwa mkewe. Kisha Mtume alisimama akiwa amechukizwa sana na akasema: "Unacheza na Kitabu cha Mwenyezi Mungu (s.w) nikiwa bado tupo pamoja (nikiwa bado s/afa)?" (Mtume alikasirika) kwa kiasi ambacho mtu mmoja alisimama akauliza: Je, siwezi kumuua? (Nisai)



Hukumu ya talaka tatu ni kwamba baada ya mume kutamka talaka ya tatu hawezi tena kumrejea mkewe katika kipindi cha eda hata kama watapatana vipi. Baada ya kipindi cha eda kwisha, mkewe atakuwa ameachika kwa talaka tatu na atakuwa huru kuolewa na mume mwingine yeyote aliyehalalishwa kwake katika sheria ya Kiislamu. Lakini ni haramu mwanamke huyo kuolewa na mumewe wa kwanza mpaka aolewe na mume mwingine. Kisha akiachika kwa mume wa pili kwa sababu za msingi au akiachwa mjane, ndipo itakuwa halali kwake kuolewa na mume wake wa kwanza. Ndoa ya namna hii inajulikana kwa jina Ia "Tahliil". Qur-an inabainisha hukumu hii katika aya ifuatayo:



Na kama amempa talaka (ya tatu) basi (mwanamume huyo) si halali kwake baada ya hapo mpaka aolewe na mume mwingine. Na (mwanamume huyo mwingine) akimwacha, basi hapana dhambi kwao kurejeana (kwa kuoana tena) wakiona kuwa watasimamisha mipaka ya Mwenyezi Mungu. Na hii ni mipaka ya Mwenyezi Mungu anayoibainisha kwa watu wajuao. (2:230)



Hukumu hii kali imetolewa iii Waislamu wasifanye mas-khara na talaka. Kuna baadhi ya Waislamu, wakikwaruzana tu kidogo na wake zao hutishia talaka au anatoa talaka kabisa. Mtu akiendelea na mchezo huu atajistukia ameshamuacha mkewe kwa talaka tatu na hana namna tena ya kumrejea. Ni katika mchezo huu wa kutoa talaka tatu bila kufikiri na kumuogopa Mwenyezi Mungu, baadhi ya Waislamu wameishia katika majuto. Baadhi ya Waislamu wanadiriki kumdanganya Mwenyezi Mungu kwa mtu kumuhonga mume mwingine amuoe mtalaka wake kwa lengo Ia kumuacha baada ya muda mfupi (na ikiwezekana asimguse) iii awe halali kuolewa na mume wake wa mwanzo. Huku ni kuzifanyia mzaha sheria za Mwenyezi Mungu na ni Haramu ya uwazi. Ndoa za namna hiyo hazisihi mbele ya Mwenyezi Mungu (s.w).



(b)Talaka ya Li'aan
Talaka hii hupatikana kwa viapo viwili cha mume na mke. Ikitokea kwamba mume au mke amemkamata mwenzie ugoni lakini hapana mashahidi wanne walioshuhudia kitendo hicho ila yeye mwenyewe itabidi, kama mume ndiye aliyemkamata mkewe ugoni, aape kwa kurudia mara nne kuwa anashuhudia kuwa mkewe mzinifu, kisha mara ya tano aape kwamba Iaana ya Mwenyezi Mungu iwe juu yake ikiwa yeye ni miongoni mwa waongo. Mke naye ataapa mara nne kujitetea kuwa yeye hakufanya kitendo hicho kisha mara ya tano aape kuwa Iaana ya Mwenyezi Mungu iwe juu yake kama mumewe ni miongoni mwa wasemao kweli. Viapo hivi vinabainishwa katika aya zifuatazo:


Na wale wanaowasingizia wake zao (kuwa wamezini) na hawana mashahidi ila nafsi zao, basi ushahidi wa mmoja wao utakuwa kushuhudilia mara nne kwa kiapo cha Mwenyezi Mungu ya kwamba: bila shaka yeye ni mmoja wa wanaosema kweli.



Na mara ya tano (aape) kwamba laana ya Mwenyezi Mungu iwe juu yake ikiwa ni miongoni mwa waongo. Na (mke) itamuondokea adhabu kwa kutoa shahada mara nne kwa kiapo cha Mwenyezi Mungu ya kwamba (mume) ni miongoni mwa waongo.



Na mara ya tano (aape) ya kwamba hasira ya Mwenyezi Mungu iwe juu yake kama (mumewe) yu miongoni mwa wanaosema kweli, (na yeye mke ndiye mwongo). (24:6-9)
Baada ya kuapizana hivi, hapo hapo ndoa itakuwa imevunjika moja kwa moja kwani wawili hawa hawategemewi tena kurejeana na kukaa kwa furaha na amani.




                   


Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 208

Post zifazofanana:-

JITIBU KWA MUAROBAINI: faida za kiafya za muarobaini
1. Soma Zaidi...

Uteuzi wa Uthman bin Al-'Afan khalifa wa Tatu baada ya Mtume
Soma Zaidi...

Yajuwe mandalizi ya Ibada ya hija
Soma Zaidi...

ilinde Afya yako
Hiki ni kitabu kilichosheheni masomo zaidi kuhusu Afya yako, vyakula pamoja na maradhi sugu. Soma Zaidi...

Hadithi ya kinyozi kaka wa pili
Soma Zaidi...

Kitabu cha Afya 03
Yajuwe mambo yanayoathiri afya ya miili yetu, jifunze mambo mengi kuhusu afya. Soma Zaidi...

HADITHI YA NURDINI 03: Mtumwa wa Gharama
Kama wasemavyo waliokula chumvi nyingi kuwa muomba mungu hachoki, basi waziri Faridi aliendelea kuomba Mungu hata siku moja akapata taarifa kuwa kuna watumwa wametokea nchi za Uajemi. Soma Zaidi...

NINI VIDONDA VYA TUMBO?
Ni vidonda vinavyotokea katika ukuta wa tumbo. Vidonda hivi tumezoea kuviita vidonda vya tumbo ila hapa nitataja kitaalamu kuwa vidonda hivi hufahamika kama peptic ulcers. Soma Zaidi...

Maana ya Mirathi na kurithi katika uislamu
Maana ya MirathiMirathi katika Uislamu ni kanuni na taratibu alizoziweka Allah (Sw) katika kuwagawawia na kuwarithisha familia na jamaa, mali aliyoiacha marehemu. Soma Zaidi...

MAANA YA HADITHI SUNNAH
Maana ya SunnahKilugha: Neno sunnah katika lugha ya Kiarabu lina maana ya mwenendo au mila. Soma Zaidi...

Kuandaliwa Mtume(s.a.w) maandalizi ya kimafunzo na maandalizi ya ki ilham
Mitume huzaliwa Mitume. Soma Zaidi...

GEOGRAPHY NECTA PAST PAPERS REVIEW PAPERR 07
242. Soma Zaidi...