Haki za kijamii za mwanamke katika uislamu

Haki za kijamii za mwanamke katika uislamu

Haki za kijamii
Pamoja na haki za kiuchumi, Uislam unampa mwanamke haki za kijamii zifuatazo:



Kwanza, mwanamke amepewa uhuru kamili wa kuolewa na mwanamume ampendaye. Ndoa ya Kiislamu haisihi iwapo mwanamke atalazimishwa kuolewa kinyume na ridhaa yake. Vile vile hapana ruhusa ya kumkataza mwanamke asiolewe na mwanamume ampendaye ndani ya mipaka ya sheria ya Kiislamu.



Pili, mwanamke amepewa haki zote za kisheria za kumuacha mumewe ambaye amekosa nguvu za kiume (impotent), ambaye ni katili kwake na ambaye anamchukia.



Tatu, mwanamume ameamrishwa kutumia madaraka aliyopewa juu ya mkewe kwa huruma na upendo. Kama Qur'an inavyoagiza:
"... basi kaeni nao kwa wema ..." (4: 19). Wala msisahau kufanyiana Ihsani baina yenu ..." (2:237).



Na Mtume (s.a.w) amesema: 'Wabora wenu ni wale walio wema kwa wake zao na watu wao (katika familia)". Kama mwanamume atatumia vibaya madaraka yake, mwanamke ana kila haki ya kukiendea chombo cha sheria na kumshitakia mumewe ambaye hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.


Nne, wanawake wajane na waliotengana na waume zao wanahaki na uhuru kamili wa kuolewa tena. Haki hii haijapatikana kwa jamii nyingi ulimwenguni.
Tano, kuna usawa kamili kati ya wanaume na wanawake kwa upande wa sheria za madai na jinai. Sheria ya Kiislamu haibagui wala haipendelei mwanamume au mwanamke katika kulinda haki za watu na haki zajamii kwa ujumla. Kwa mfano hukumu ya Kiislamu kwa mwizi ni kukatwa mkono, awe mwanamume au mwanamke kama inavyobainishwa katika Qur'an;


Na mwizi mwanamume na mwizi mwanamke, ikateni mikono yao, malipo ya yale waliyoyachuma. Ndiyo adhabu itokayo kwa Mwenyezi Mungu. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu na Mwenye He/dma (5:38).



Kuhusu adhabu ya wazinifu tunafahamishwa: Mzinfu mwanamke na mzinfu mwanamume mpigeni kila mmoja katika wao mj/eledi mia. Wala isiwashikeni kwa ajili yao huruma katika kupitisha hukumu hii ya Mwenyezi Mungu, ikiwa nyinyi mnamuamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho. Na lishuhudie adhabu hiyo kundi la Waislam. (24:2).
Sita, vile vile wanawake nao kama wanaume wanaruhusiwa kutoa ushahidi mahakamani au pale ushahidi wao unapohitajika. Bali katika kipengele hiki itatubidi tuwe wazi kwa kujibu maswali mbali mbali yanayoweza kuulizwa kama vile:


Kwa nini wanatakiwa mashahidi wawili wanawake badala ya shahidi mmoja mwanamume? Je, hii ma maana kuwa Uislamu unamhesabu mwanamke kuwa ni nusu ya mwanamume? La! Hasha. Kama katika suala Ia urithi, ukitazama kwa sura ya nje unaweza kudhani kuwa mwanamke ameonelewa na mwanamume kapendelewa kwa mwanamume kupewa mara mbili ya mwanamke. Hivyo hivyo katika suala Ia ushahidi, kwa kutakiwa wanawake wawili haina maana kuwa Uislamu unamuona mwanamke kuwa ni nusu ya mwanamume. Lau ingekuwa hivyo, Uislam ungeweza kuukataa ushahidi wake moja kwa moja. Na katika karne ya 7A.D iliposhuka Qur'an hata huko kuukubali ushahidi wa mwanamke kulionekana ni kioja na kuruka mipaka.


Na mshuhudishe mashahidi wawili katika watu wenu wanaume. Lakini ikiwa hakuna wanaume wawili, basi mwanamume mmoja na wanawake wawili; katika wale mnaowakubali kuwa mashahidi. Ili kama mmoja wao akipotea, mmoja wao amkumbushe mwingine "(2:282).



Ushahidi unaotajwa katika aya hii unahusiana na mikataba ya mambo ya fedha. Mashahdi wanatakiwa wawe ama wanaume wawili au mwanamume mmoja na wanawake wawili. Na sababu ya kuwaweka wanawake wawili imetajwa nayo ni kuwa akisahau mmoja mwenzake atamkumbusha. Swali Ia kujiuliza hapa ni kuwa kwa nini ihofiwe kuwa mwanamke ndiye atakayesahau na siyo mwanamume? Tatizo lililopo hapa kwa kiasi fulani linatokana na kasoro za kutafsiri neno "tadhila" kama kusahau. Neno "tadhila" halina maana ya kutokuwa na kumbukumbu (memory). Kwani mara nyingi wanawake hukumbuka zaidi kumbukumbu zao za kuzaliwa kuliko hata wanaume. Katika Uislam mwanamke ambaye kwa kawaida atakuwa anatimiza majukumu yake kama mke au mama aweza kujishughulisha na hayo kiasi Cha kumfanya asiwe hadhiri sana wakati wa majadiliano yanayohusu kuandikiana mikataba ya masuala ya fedha, masuala ambayo hahusiki nayo mara kwa mara.


Hii ni kwa kawaida, lakini haina maana kuwa kila mwanamke lazima atakuwa hivyo. Hata hivyo kwa sababu lengo Ia sheria ni kulinda haki za watu, sheria imeweka hadhri hiyo iii kuhakikisha kuwa haki za watu zinahifadhiwa. Na lengo si kumdhalilisha mwanamke. Kwani Iau ushahidi wa mwanamke ungekuwa unakataliwa tu kwa sababu mwanamke ni kiumbe dhalili basi Hadith zilizopokewa kutoka kwa wanawake zingekataliwa. Lakini Hadith zilizopokewa kutoka kwa Bibi Aisha kwa mfano ni sehemu ya msingi wa sheria yenyewe. Ni upi ushahidi mzito zaidi, wa kupokea Hadith au wa kuandikishiana mikataba ya pesa? Yote hayo yanaonesha kuwa lengo ni kuhifadhi haki za watu zisipotee kwa sababu ya kughafilika na siyo kumdunisha mwanamke.




                   




Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 134


Download our Apps
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Mbinu za Da'wah Alizotumia Nuhu(a.s)
Katika kufikisha ujumbe huu kwa watu wake Nuhu(a. Soma Zaidi...

Sifa za wanafiki zilizotaja katika surat An-Nisaa (4:60-63, 88, 138-145)
Huwaoni wale wanaodai kwamba wameamini yale yaliyoteremshwa kwako na yaliyoteremshwa kabla yako? Soma Zaidi...

Masiku ya Tashiq, kuchinja na kufanya tawafu ya kuaga
8. Soma Zaidi...

Haki, wajibu na majukumu katika familia ya kiislamu na majirani zake
Soma Zaidi...

MAANA YA Quran
Maana na majina ya Quran Maana ya Wahyi. Soma Zaidi...

Lengo la swala
Lengo la Kusimamisha SwalaBila shaka swala imepewa umuhimu mkubwa kiasi cha kufanywa nguzo kubwa ya Uislamu kutokana na lengo lake. Soma Zaidi...

jamii muongozo
Haja ya Mwongozo kutoka kwa Allah (s. Soma Zaidi...

Hadhi na Haki za Mwanamke Katika Jamii
Soma Zaidi...

(c)Vipawa vya Mwanaadamu
Vipawa vya mwanaadamu ni sababu nyingine inayomfanya mwanaadamu asiweze kuishi bila ya kufuata dini moja au nyingine. Soma Zaidi...

Mtazamo na Msimamo wa Uislamu Juu ya Kudhibiti Uzaz (uzazi wa mpango) na hukumu yake
Soma Zaidi...

Nini maana ya Uchoyo, na madhara yake kwenye jamii
31. Soma Zaidi...

Nini maana ya Husda, na ni yapi madhara yake
34. Soma Zaidi...